Kombe la Dunia: Marekani yatetea bango la wachezaji wa Argentina

Chanzo cha picha, Getty Images
Ikulu ya Marekani imetetea timu ya taifa ya Argentina baada ya wachezaji wake kuonyesha bango lililoandikwa "Las Malvinas son Argentinas" ("Visiwa vya Falklands ni vya Argentina") kufuatia ushindi wao dhidi ya England katika nusu fainali ya Kombe la Dunia.
Hatua hiyo imekosolewa na Uingereza huku Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) likitatarajiwa kuchukua hatua za kinidhamu.
Andrew Giuliani, mkuu wa kikosi kazi cha FIFA cha Ikulu ya Marekani, amesema wachezaji hao walikuwa wakitumia haki yao ya uhuru wa kujieleza chini ya Marekebisho ya Kwanza ya Katiba ya Marekani walipokuwa nchini humo, kwa mujibu wa BBC.
Bango hilo linarejelea madai ya muda mrefu ya Argentina kuhusu visiwa vilivyoko kusini mwa Bahari ya Atlantiki, vinavyojulikana kwa Kiingereza kama Falkland Islands na kwa Kihispania kama Las Malvinas.
Serikali ya Uingereza imekosoa kitendo hicho, huku Ikulu ikisisitiza kwamba Visiwa vya Falklands "kwa hakika ni" vya Uingereza na kuunga mkono wito wa FIFA kuchunguza iwapo bango hilo lilikiuka kanuni za shirikisho hilo zinazokataza kauli za kisiasa wakati wa mechi.
Serikali ya Visiwa vya Falklands pia imeeleza kusikitishwa kwake na kuitaka FIFA kuichukulia hatua timu ya Argentina, ikisema haitaki kutumiwa kama "mpira wa kisiasa".
Soma Zaidi:





















