Iran yatangaza likizo ya umma ili kujiandaa kwa mazishi ya Khamenei

Chanzo cha picha, Getty Images
Serikali ya Iran imetangaza Jumanne, Julai 6, kuwa siku ya mapumziko ya umma mjini Tehran.
Msemaji wa serikali ya Iran, Fatima Mohajerani, amesema hatua hiyo inalenga kuwezesha waombolezaji wa kiongozi wa zamani wa Iran kurejea kutoka mji mkuu.
Pia amesema siku ya maombolezo ya kitaifa itaadhimishwa nchini Iran siku ya Alhamisi, huku mazishi ya Ali Khamenei yakitarajiwa kufanyika mjini Mashhad Julai 8.
Kwa mujibu wa ratiba rasmi, sala za mazishi na shughuli za kuaga mwili wa Khamenei zitafanyika kati ya Julai 4 na 8 katika miji ya Tehran, Qom na Mashhad. Hafla za kutoa pole pia zitafanyika katika miji ya Baghdad, Kazmin, Karbala na Najaf nchini Iraq.
Inakumbukwa kuwa Ali Khamenei aliuawa katika mashambulizi ya anga ya Marekani na Israel dhidi ya Iran yaliyolenga makazi na ofisi yake, maarufu kama Nyumba ya Uongozi, lakini hadi sasa bado hajazikwa.
Unaweza kusoma;





















