Mwanaharakati Kemi Seba akamatwa Afrika Kusini kwa kuchochea mapinduzi nchini Benin

Chanzo cha picha, Anadolu via Getty Images
Maafisa wa polisi Afrika Kusini wanasema kuwa wamemkamata “mtoro” ambaye ni mwanaharakati wa Benin aliyekuwa akitafutwa.
Kemi Seba, anasemekana alikuwa akijaribu kukimbilia ulaya kupitia Zimbabwe.
Seba ambaye jina lake kamili ni Stellio Gilles Robert Capo Chichi, anatafutwa na mamlaka nchini Benin “kwa kuchochea uasi” baada ya kuunga mkono mapinduzi ya serikali yaliyotibuka mwaka uliopita.
Mwanaharakati huyo alikamatwa siku ya Jumatatu na mwanawe kijana mwenye umri wa miaka 18 mjini Pretoria. Mtu aliyekuwa amelipwa kuwasaidia kuenda nchini Zimbabwe, pia anazuiliwa na polisi.
Seba mwenye umri wa miaka 45, anajulikana kwa kupinga ushawishi wa Ufaransa barani Afrika.
Kemi Seba alizaliwa nchini Ufaransa na wazazi wake ni wazaliwa wa Benin na anawafuasi zaidi ya millioni 1.5 kwenye mitandao ya kijamii.
Amehukumiwa mara kadhaa nchini Ufaransa kwa kuchochea chuki, ukabilia na chuki dhidi ya wayahudi.
Mwaka wa 2024, alinyanganywa uraia wake wa Ufaransa, na akajibu hatua hiyo kwa kuchoma pasipoti yake hadharani na kusema kuwa “amekombolewa kutoka kwa kubeba mzigo wa kuwa raia wa Ufaransa.”
Pia unaweza kusoma:













